给橙子写的一首斯瓦希里语诗

CHENZA
1
Chenza kwetu kawaida,
  Vichochoro lauzika,
Nikila kama ziada,
  Fukuto nalo lashuka,
Ikiwa kinga ni mada,
  Kiseyeye chazimika,
Chenza huliwa na nani,
  Walimaji hawajali.

2
Chenza tunda la magwanda,
  Moja bei chini Kwacha,
Alilaye hulipenda,
  Hatosheki kuliacha,
Lilwao watu na kenda –
  Wanyama wenye makucha,
Chenza huliwa na nani,
  Walimaji hawajali.

3
Chenza pia lasafiri,
  Wapi na wapi lendapi?
Ilivyo kubwa bahari,
  Nani afunga halapi?
Hwenda Mamanga hodari,
  Tena Wareno wafupi,
Chenza huliwa na nani,
  Walimaji hawajali.

4
Chenza pia ana ndugu,
  Limau ‘sinilaumu,
Hizaya, chira na sugu,
  Kula ‘furutu ni sumu,
Ila dawa ya mabugu,
  Mvinyo mwa mlizamu,
Chenza huliwa na nani,
  Walimaji hawajali.

5
Chenza ‘kawa na mtoto,
  Jina kupewa ni chungwa,
Chungwa ladhaye kitoto,
  Aloshiki’ya Mwanangwa,
Ningampa maguruto,
  Hofu sana longwalongwa,
Chenza huliwa na nani,
  Walimaji hawajali.

6
Chenza visa kuumana,
  Mlimwengu nakwambia,
Kwamba langu kubwa mbona?
  Jeuri ‘liulizia,
Jawabu kwa kweli sina,
  Tabia nchi na mwia,
Chenza huliwa na nani,
  Walimaji hawajali.

7
Chenza ‘lojali ni nini,
  Hata mie silijui,
Sinini wala sinini,
  Bora pia hutambui,
Mdau awe chomboni,
  Pasipo pepo hashui,
Chenza huliwa na nani,
  Walimaji hawajali.

na Mroho Sinini
—–
CHENZA / 橙子~ 橙仔 [tʂəŋtsɑ]

 

ynshen