https://www.facebook.com/187353645175928/videos/410301496947059
下载:HusseinIssaTuwa&ITV
[KUNAKILI KUANZIA 00:53]
Moderater (baadae kwa kifupisho cha M): Hussein Tuwa karibu sana hapa ITV. Hapa inaonyesha kwamba wewe ni Rais wa UWARIDI. UWARIDI kwa maana ya nini? UWARIDI ni kitu gani?
Hussein (baadae kwa kifupisho cha H): Mimi ni urais wa UWARIDI ambao ni umoja wa waandishi wa riwaya wenye dira Tanzania.
M: Umoja wa waandishi wa riwaya wenye dira?
H: Unajua UWARIDI kuna waandishi wa riwaya halafu kuna waandishi wa riwaya wenye dira kuna tofauti yale. Sasa sisi kwenye UWARIDI tumejipambanua kwamba tunafanya uandishi wa riwaya lakini kwa malengo mahsusi ya kuisogeza kwanza fasihi ya Tanzania mbele, kuiweka juu ionekane lakini vile vile nasisi waandishi wenyewe tuweze kunufaika kwa kazi za mikono yetu kwahiyo tunavofanya vitu tunakwenda kwa malengo tunakuwa tuna dira maalum ya kutuongoza. siyo tunaandika, kwa waandishi miongoni mwa waandishi tu hapana ni waandishi wenye dira tunaandika kwa malengo, tunaandika kwa ueledi, tunaandika kwa kufuata maadili, tunaandika kwa kuwa na utaratibu mahsusi ambao tunaamini tukifuata ule utaratibu tutafika kule tutakapofika, au tutafikisha fasihi ya Tanzania kule inapopaswa iwe.
